SIMBA YAUTAFUNA MFUPA WA TANGA ULIOWASHINDA AZAM NA YANGA


SIMBA YAUTAFUNA MFUPA WA TANGA ULIOWASHINDA AZAM NA YANGA
Wachezaji wa Simba wakimpongeza Hamisi Kiiza baada ya              kufunga baon la pili na la ushindi dhidi ya Coastal Union              kwenye uwanja wa Mkwakwani
Wachezaji wa Simba wakimpongeza Hamisi Kiiza baada ya kufunga baon la pili na la ushindi dhidi ya Coastal Union kwenye uwanja wa Mkwakwani

Magoli mawili kutoka kwa Danny Lyanga na HamisI Kiiza yameipa Simba ushindi wa tatu kwenye uwanja wa Mkwakwani msimu huu na kuondoka na pointi zote tisa kwa kuzifunga timu za Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani na kuendelea kutamalaki kileleni mwa ligi na sasa imefikisha jumla ya pointi 57 baada ya kucheza michezo 24 ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Mshambuliaji wa Simba na mfungaji wa goli la kwanza              Danny Lyanga akipambana na beki wa Coastal Union
Mshambuliaji wa Simba na mfungaji wa goli la kwanza Danny Lyanga akipambana na beki wa Coastal Union

Mchezo hakuwa rahisi kwa Simba licha ya kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 mbele ya Coastal Union ambayo inakamata mkia kwenye ligi kutokana na kukumbana na upinzani mkali kutoka kwa 'wagosi wa kaya' ambao walishindwa kupata mabao licha ya kupata nafasi kadhaa za kufunga.

Danny Lyanga aliifungia Simba goli la kwanza dakika ya 39 kipindi cha kwanza kisha Kiiza akamaliza kazi dakika ya 51 na kupeleka shangwe kwenye mtaa wa Msimbazi.

Mashabiki wa Simba waliofurika uwanja wa Mkwakwani              wakishangilia goli la kwanza lillilofungwa na Danny Lyanga
Mashabiki wa Simba waliofurika uwanja wa Mkwakwani Tanga, wakishangilia goli la kwanza lillilofungwa na Danny Lyanga

Takwimu na rekodi muhimu

  • Simba imezifunga timu zote za Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani msimu huu ikianza kushinda kwa bao 1-0 mechi yake ya ufunguzi wa ligi dhidi ya African Sports kisha kuifunga Mgambo JKT na kumaliza na Coastal Union.
  • Simba imepata pointi 6 dhidi ya Coastal Union msimu huu baada ya kushinda mechi zote mbili za ligi dhidi ya timu hiyo ya Tanga, Simba iliifunga Coastal kwenye mchezo wa awali kwenye uwanja wa taifa kisha leo kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Mwamuzi wa mchezo kati ya Coastal Union dhidi ya Simba              akiokota chupa za maji zilizokuwa zikirushwa na mashabiki wa              Simba waliokuwa wakipinga maamuzi ya mwamuzi msaidizi (line              one)
Mwamuzi wa mchezo kati ya Coastal Union dhidi ya Simba akiokota chupa za maji zilizokuwa zikirushwa na mashabiki wa Simba waliokuwa wakipinga maamuzi ya mwamuzi msaidizi (line one)
  • Wachezaji watatu wa zamani wa Simba wanaocheza Coastal Union walikuwa wakikutana na timu yao ya zamani (Abdulahim Humoud, Ibrahim Twaha na Ally Shiboli.
  • Kocha wa Simba Jackson Mayanja alikuwa anakutana na Coastal Union kwa mara ya kwanza tangu aondoke baada ya kuchukuliwa na Simba. Mayanja ameiongoza Simba kushinda mechi 10 kati ya 11 za ligi
Beki wa kushoto wa Simba Mohamed Hussein 'Tshabalala'              akimtoka beki wa Coastal Union
Beki wa kushoto wa Simba Mohamed Hussein 'Tshabalala' akimtoka beki wa Coastal Union wakati akipandisha kushambulia
  • Hamisi Kiiza amefunga bao lake la 19 kwenye ligi msimu huu na kumwacha mpinzani wake wa karibu Amis Tambwe kwa magoli mawili.
  • Simba sasa inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya wapinzani wake kwenye mbio za ubingwa Yanga na Azam zenye pointi 50 kila moja huku zikiwa zimecheza mechi 21 mechi tatu nyuma ya Simba.
Mashabiki wa Simba kutoka kundi la 'Simba Makini'              wakishangilia ushindi wa timu yao kwenye uwanja wa Mkwakwani              mara baada ya kumalizika kwa mchezo
Mashabiki wa Simba kutoka kundi la 'Simba Makini' wakishangilia ushindi wa timu yao kwenye uwanja wa Mkwakwani mara baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Coastal Union dhidi ya Simba


Comments