PICHA 60: MHE. NAPE NNAUYE ALIPOKUTANA NA WANAMUZIKI WA DANSI NA KUAHIDI KUREJESHA MUZIKI WA DANSI …ataka vyama vya muziki vijisafishe, aahidi kuifumua Cosota



PICHA 60: MHE. NAPE NNAUYE ALIPOKUTANA NA WANAMUZIKI WA DANSI NA KUAHIDI KUREJESHA MUZIKI WA DANSI …ataka vyama vya muziki vijisafishe, aahidi kuifumua Cosota

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Mheshimiwa Nape Nnauye Jumatatu mchana alikutana na wadau na wanamuziki wa dansi katika ukumbi wa Vijana Social Kinondoni  jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo mkubwa, Nape alisikiliza kero mbali mbali za wasanii wa muziki wa dansi na kuahidi kuwa atapambana kurejesha heshima ya muziki wa dansi.

Pamoja na kujibu hoja mbali mbali za wanamuziki wa dansi, Nape akaamuru iundwe kamati ya watu 11 itakayowasaliana naye maja kwa moja katika kutafuta njia nzuri ya kutatua  baadhi ya kero na baadae kupeleka mrejesho kwa wanamuziki.

Nape akasema  kamati hiyo itakuwa ni kiunganishi cha muda kati yake na wanamuziki wa dansi.

Miongoni mwa mambo aliyoahidi Nape ni pamoja na kuzipunguzia bendi kodi zisizo na lazima wakati zinapofanya maonyesho yao kwenye kumbi mbali mbali.

Nape aliyekuwa akishangiliwa mara kwa mara na wanamuziki, akaahidi pia kuifumua COSOTA (Chama cha Hatimiliki) pamoja na kuvisafisha vyama vya muziki kikiwemo Chamudata.

"Hatutasaidia chama chochote kabla ya kuvisafisha," alisema Nape na kushangiliwa kwa nguvu hasa pale alipoongeza: "Vyama hivi vinaonyesha vina walakini na ndio maana wanamuziki wengi hawavifuati."

Waziri huyo wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pia akaahidi kuwakutanisha wanamuziki wa dansi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli.

"Nitahakikisha muziki wa dansi unarejesha heshima yake, muziki wa dansi ndiyo muziki wa ukweli lakini wanamuziki wake wanakufa masikini," alisema Nape ambaye pia alihidi kurejesha matamasha na mashindano ya muziki wa dansi.

Moja ya kero kubwa na iliyolalamikiwa sana kwa Mheshimiwa Nape ni suala la bendi kutakiwa kumaliza maonyesho yao saa 6 za usiku, jambo aliloahidi kulishughulikia.

"Hili lipo kwa mujibu wa sheria, lakini tutaangalia namna ya kulitatua maana kwa kweli watu wengi wanaokwenda dansi wanaingia ukumbini saa 6 za usiku, sasa unapotaka muda huo ndiyo muziki uzimwe inakuwa ni tatizo," alitiririka Mheshimiwa Nape.

Baadae Nape aliyekuwa akiongea mbele ya vingozi wa Shirikisho la Muziki la Vyama vya Muziki Tanzania, CHAMUDATA (Chama Cha Muziki wa Dansi Tanzania) na BASATA (Baraza la Sanaa la Taifa), akataja majina ya kamati ya watu 11 aliotaka iundwe.

Nape akataka yeyote mwenye tatizo na mjumbe yeyote wa kamati hiyo iliyopendekezwa na viongozi wa Shirikisho la Muziki la Vyama vya Muziki Tanzania, Chamudata na Basata, aseme na ataondolewa.

Miongoni mwa majina yaliyounda kamati hiyo ni Waziri Ali, Hamza Kalala, Kida Waziri, Asha Baraka, Ally Chocky, Abdallah Mgonahazilu, Edna Pambamoto, Said Mdoe na Hassan Msumari (Katibu wa Chamudata) ambaye wanamuziki walilipinga jina lake na nafasi yake ikachukuliwa na Khalid Chokoraa.

Zifuatazo ni picha 60 za mkutano huo wa Mheshimiwa Nape na wanamuziki wa dansi.
 Mheshimiwa Nape akisikiliza hoja za wanamuziki wa dansi
 Mwanamuziki mkongwe Abuu Omar
 Nyoshi akisalimiana na Asha Baraka
 Shaaban Dede akitoa hoja
 Hassan Msumari katibu wa CHAMUDATA
 Wanamuziki wakisimama pale Nape alipowasili ukumbini
 Hussein Jumbe
 Jado FFU
 Ally Jamwaka wa Sikinde
 Edna Pambamoto na William Kaijage
 Mwimbaji wa Kalunde Band
 Matei na Kanku Kelly
 Francis Kaswahili na Anna Mwaole
 Dephin Mununga na Keppy Kiombil
 Nyoshi na Khalid Chokoraa
 Khamis Dacota na Chaz Baba
 Juma Mbizo na Said Kibiriti
 Kida Waziri "Stone Lady" na Asha Baraka "Iron Lady"
 John Kitime akiandaa vidokezo muhimu
 Wanamuziki wakongwe wakimsikiliza Nape

 Malu Stonch wa FM Academiaa
 Mama Kitenge (kushoto) na Edna Pambamoto
 Nyoshi na Hamza Mapande "Dogo White" wa Twanga Pepeta
 Adoplh Mbinga na Hajj BSS wa Twanga Pepeta (kulia)
 Waziri Ali wa Njenje (kushoto) akiwa na Abdul Misambano wa TOT
 Mjusi Shemboza wa Sikinde (kushoto) na Bonphace Kachele
 Mule Mule FBI wa BMM Band na Balatee wa FM Academia
 Kushoto ni mwimbaji Liston Maina
 Mwinjuma Muumin na mwandishi Khadija Khalili
 Mzee Makassy (kushoto) akimsikiliza Nape kwa makini
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Mheshimiwa Nape Nnauye akizungumza na wanamuziki wa dansi
 Mheshimiwa Nape akisisitiza jambo
 Marlon Linje na Innocent Nganyagwa
 Ado November rais wa Shirikisho la Vyama vya Muziki Tanzania
 Wanamuziki wengi walijitokeza
 Nyoshi el Saadat kiongozi wa FM Academia
 Patcho Mwamba na Totoo Ze Bingwa nao walikuwepo
 Kulia ni Rashid Pembe
 Mwanahabari Peter Mwendapole
 Dekanto Bass (kushoto) na Pitchou Meshaa wote kutoka Akudo
 Mpiga solo Rama Karenga
 Rama Pesambili meneja wa Akudo Impact
 Mwimbaji Hassan Rehani Bitchuka
 Rogart Hegga na Ally Chocky
 Mwimbaji Roshy Mselela
 Bosi wa Ruby Band
 Mwanamuziki mkongwe Salum Zahoro
 Kushoto ni Ally Star wa TOT
 Maria mdau wa muziki wa dansi kutoka Italia (kushoto) akiwa na mtangazaji Mwinyiami Maftah "Stazo"
 Kushoto ni Taji Mbaraka
 Nape akiwa meza kuu na viongozi wa Basata, Chamudata na shirikisho la muziki
 Jimmy Chika mhariri wa Dimba
 Waandishi wa habari
 Wadau na wanamuziki wakimsikiliza Nape
 Ally Chocky na Adolph Mbinga
 Wanamuziki waliofurika Vijana Social Hall
William Kaijage




Comments