KAMA ULIIKOSA RATIBA YA ROBO FAINALI YA CHAMPIONS LEAGUE TUPIA MACHO HAPA


KAMA ULIIKOSA RATIBA YA ROBO FAINALI YA CHAMPIONS LEAGUE TUPIA MACHO HAPA

Zlatan Ibrahimovic and            PSG lie in wait for Manchester City after they beat Chelsea in            the last 16

YAMETIMIA… Hatimaye ratiba ya robo fainali ya Champions League imetoka huku miamba pekee ya England iliyobaki katika michuano hiyo, Manchester City ikiangukia mikononi mwa Paris Saint-Germain (PSG).

City inacheza kwa mara ya kwanza hatua hiyo, lakini kocha wake, Manuel Pellegrini tayari ameonja ladha yake akiwa na Villarreal na Malaga, na ana matumaini ya kujiandikia historia ya kufuzu nusu fainali kabla ya kumwachia mikoba Pep Guardiola mwisho wa msimu.

Katika ratiba hiyo, Bayern Munich itakwaana na Benfica, Wolfsburg na Real Madrid, huku Atletico Madrid ikipewa Barcelona katika vita ya miamba ya ligi moja.

Mechi za awali za hatua hiyo zitapigwa Aprili 5-6 na marudiano April 12-13

Comments