Harry Kane aifikia rekodi ya ufungaji ya Alan Shearer Iliyodumu kwa miaka 20


Harry Kane aifikia rekodi ya ufungaji ya Alan Shearer Iliyodumu kwa miaka 20

HARRY KANE ametengeneza historia mpya jana jumapili katika ligi kuu ya Uingereza. 

01_21092602_e41bb7_2753134aAmekuwa mchezaji wa kwanza wa Spurs katika kipindi cha miaka 44 kufunga magoli 20 au zaidi katika misimu miwili mfululizo. Shujaa wa Tottenham Martin Chivers alifunga magoli 21 ya ligi katika msimu wa 1970-71 na akafunga magoli 25 msimu uliofuatia.

Na Harry Kane amefuata nyayo zake kwa magoli mawili aliyofunga dhidi ya Bournemouth  @White Hart Lane ambayo yamefanya atimize magoli 21, idadi sawa na ya msimu uliopita.

Kane alisema: Nina furaha sana na ushindi wa 3-0, ushindi mzuri kuelekea break ya mechi za kimataifa."

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England sasa anaungana na listi ya wachezaji wa Uingereza ambao waliweka rekodi kama yake. 02_21092602_3b8b03_2753132aKane ndio mchezaji wa kwanza wa England tangu Alan Shearer mwaka 1997 kufunga magoli 20 au zaidi kwa misimu miwili mfululizo.

Harry Kane anakuwa mchezaji wa tano wa England katika historia ya Premier League Shearer, Robbie Fowler, Les Ferdinand na Andy Cole kuwa na rekodi ya kufunga magoli 20 au zaidi katika misimu miwili mfululizo.

 



Comments