ZINEDINE ZIDANE            ameweka wazi kuwa yeye ni shabiki wa Leicester City na              kusema kuwa itakuwa jambo la kusisimua kuwaona katika Champions League              msimu ujao.
        Baada ya kunusurika              kushuka daraja msimu uliopita, Leicester City              wamecharuka msimu huu na sasa wanaongoza msimamo wa Ligi Kuu              ya England huku zikiwa zimesalia mechi 12.
        Na kwa mujibu wa              kocha huyo wa Real Madrid, kiwango cha Leicester City              kimeishtua bara zima la Ulaya.
        Zidane anasema:            "Katika hatua hii ya ligi, Leicester kuwa kileleni ni mafanikio              yaliyotukuka.
        "Wamekuwa gumzo sio England              pekee bali Ulaya nzima. Kukiwa na timu zenye majina makubwa              England na pesa za kumwaga, wakifanikiwa kutinga Champions              League itakuwa ni jambo la kipekee katika soka."
        
Comments
Post a Comment