CHELSEA imemuongeza kiungo Mjerumani wa            Real Madrid, Toni Kroos katika listi ya mastaa inaowafukuzia            kiangazi hiki, ingawa italazimika kuvunja benki na kulipa            pauni milioni 234 ili ikidhi mahitaji ya mkataba wake kwa            mujibu wa mtandao wa Football Leaks.
        Mtandao wa intaneti wa Calciomercato wa            Italia, umedai kuwa Kroos mwenye umri wa miaka 25 ameingia            kwenye rada za Chelsea ambayo inahaha kusuka kikosi chake upya            baada ya kupoteza mwelekeo msimu huu.
        Mmiliki wa Roman Abramovich anapanga            kutumia kiasi kikubwa cha fedha kuirudisha klabu yake katika            mwelekeo sahihi baada ya kuonekana dhahiri kufeli kutetea taji            lake la Premier League msimu huu.
        Kroos aliyejiunga na Real Madrid akitokea            Bayern Munich mwaka 2014, ana mkataba Bernabeu hadi 2020,            lakini Abramovich anaweza kuonyesha 'jeuri ya fedha' na            kumng'oa staa huyo.
        
Comments
Post a Comment