KOCHA TIMU YA TAIFA ITALIA AHUSISHWA NA SAFARI YA CHELSEA KUMRITHI MOURINHO


KOCHA TIMU YA TAIFA ITALIA AHUSISHWA NA SAFARI YA CHELSEA KUMRITHI MOURINHO

GAZETI la michezo la Italia, La Gazzetta dello Sport, limeripoti kuwa Chelsea imefikia makubaliano ya awali na kocha Mtaliano, Antonio Conte kuchukua nafasi ya Guus Hiddink kiangazi hiki.

Conte mwenye umri wa miaka 46 kwa sasa ni kocha wa timu ya taifa ya Italia, lakini kwa mujibu wa La Gazzetta dello Sport, anatarajiwa kwa kiasi kikubwa kuachia ngazi wakati mkataba wake utakapofika ukomo baada ya michuano ya Euro 2016.

Safari ya kiungo huyo wa zamani wa Juventus kwenda Premier League itamfanya kuwa kazi yake ya kwanza nje ya Italia.

Huko nyuma, Conte aliajiriwa na klabu mbalimbali za Serie A zikiwamo Atalanta, Siena na Juve kabla ya kuchukua kazi ya kukinoa kikosi cha Italia – Azzurri mikononi mwa Cesare Prandelli na kukiwezesha kufuzu kwa Euro 2016 bila kupoteza mchezo.

Wakati La Gazzetta dello Sport likiripoti kufikiwa kwa makubaliano ya awali, Express Sport linabainisha kuwa Diego Simeone, Jorge Sampaoli na Massimiliano Allegri pia wapo kwenye foleni ya kuingia Stamford Bridge kumbadili Hiddink anayeiongoza Chelsea kwa muda.


Comments