JUVENTUS ALMANUSURA KWA BAYERN MUNICH ...yatanguliwa 2-0, yachomoa zote


JUVENTUS ALMANUSURA KWA BAYERN MUNICH ...yatanguliwa 2-0, yachomoa zote

JUVENTUS imenusurika kulala nyumbani baada ya kutanguliwa 2-0 na Bayer Munich lakini ikachomoa na kuambulia sare ya 2-2 kwenye mchezo wa Champions League hatua ya 16 bora.

Miamba hiyo ya Italia iliyocheza fainali dhidi ya Barcelona msimu uliopita, ilikwenda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao moja lililofungwa na Thomas Muller dakika ya 43.

Dakika ya 55 Arjen Robben akaiandikia Bayern Munich bao la pili na matokeo yakabaki hivyo hadi dakika ya 63 pale Paulo Dyabala alipoifungia Juventus goli la kwanza.

Dakika ya 76 Stefano Sturaro akaingia kwenye box na kumzidi maarifa Joshua Kimmich kabla ya kumchambua kipa Manuel Neuer na kuisawazishia Juventus.

JUVENTUS XI: Buffon; Lichtsteiner, Bonucci, Barzagli, Evra; Cuadrado, Khedira (Sturaro 69), Marchisio (Hernanes 46), Pogba; Dybala (Morata 75), Mandzukic


BAYERN MUNICH XI: Neuer; Lahm, Kimmich, Alaba, Bernat (Benatia 74); Robben, Muller, Vidal, Thiago, Costa (Ribery 84); Lewandowski.
Thomas Muller roars with celebration after putting                Bayern Munich into the lead on the stroke of half-time
Thomas Muller akishangilia baada ya kuifungia Bayern Munich bao la kwanza muda mfupi kabla ya mapumziko
Arjen Robben wheels              away in celebration after superbly firing Bayern Munich into              a two-goal lead
Arjen Robben anaiandikia Bayer Munich bao la pili
Paulo                Dybala grabs the ball as he celebrates his second-half                goal as Juventus came from two goals down
Paulo Dybala anashangilia baada ya kuipatia Juventus bao la kwanza
Stefano Sturaro beats Joshua                  Kimmich to the ball to grab an unlikely equaliser                  against Bayern Munich 
Stefano Sturaro anamzidi maarifa Joshua Kimmich na kuifungia Juventus bao la kusawazisha










Comments