MANCHESTER City inapewa nafasi kubwa ya            kuzipiga kumbo Barcelona na Juventus katika mbio za kuwania            saini ya kiungo wa Borussia Dortmund, Ilkay Gundogan.
        Mkataba wa staa huyo mwenye miaka 25            utafikia mwisho Westfalenstadion mwishoni mwa mwaka 2017,            lakini kwa mujibu wa gazeti la SPORT, tayari ameipasha            Dortmund kwamba atajiunga na City kiangazi hiki.
        Kocha ajaye Etihad, Pep Guardiola, anataka            mchezaji wa kiungo kuwa usajili wake wa kwanza, na inaonekana            kwamba turufu yake itaangukia kwa Gundogan.
        Kwa kupika mabao mawili na kufunga moja            katika mechi 20 za Bundesliga msimu huu, mashabiki wa City            wana matumaini kwamba kiungo huyo wa kimataifa wa Ujerumani            anaweza kuwa bora zaidi kama ilivyo kwa Fernando na            Fernandinho katika dimba la kati.
        
Comments
Post a Comment