GABRIEL PAULISTA ASEMA DAWA YA MESSI, NEYMAR NA SUAREZ IKO JIKONI



GABRIEL PAULISTA ASEMA DAWA YA MESSI, NEYMAR NA SUAREZ IKO JIKONI
Gabriel Paulista            (left) has been called into the Brazil squad for the upcoming            World Cup qualifiers

BEKI wa Arsenal, Gabriel Paulista (pichani kushoto) amesema kuwa wana mipango ya siri itakayowasaidia usiku wa leo kuwadhibiti wauaji watatu wa Barcelona - Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar ambao kwa pamoja wamepiga mabao 91 msimu huu, lakini akasisitiza kwamba itabaki kuwa siri hadi hapo mechi itakapoanza.

The Gunners hawapewi nafasi kubwa ya kushinda pamoja na kuwa nyumbani Emirates leo, lakini wanajua kwamba wanahitaji kupata matokeo muhimu katika mechi hii ya awali ya Champions League hatua ya 16 bora kama wanataka kuwa na nafasi ya kusonga robo fainali.

Gabriel  ambaye hatarajiwi kucheza leo kutokana na kuwa majerehi alisema: "Najua fomula ya kuwazuia Messi, Neymar na Suarez lakini imefungwa kwa kufuli saba! Siwezi kuitangaza fomula. Kama nitaitangaza, nitakuwa nahatarisha mikakati yote ya timu iliyofanyiwa kazi. Lakini haitakuwa rahisi kuwazuia."


Beki huyo aliongeza kuwa wachezaji wote wanataka kuandika Historia Arsenal, kwamba wanataka kushinda Champions League na pia Premier League.



Comments