MANCHESTER United walikataa                kufungua mlango kwa kiungo nyota wa Bayern Munich raia wa                Chile, Arturo Vidal, hali ambayo imewapa mwanya Chelsea                kufanya mazungumzo nae.
        Meneja wa Ufundi wa Chelsea,                Michael Emenalo amelazimika kusafiri hadi Italia kuangalia                pambano kati ya Bayern Munich dhidi ya Juventus ambalo                limemalizika kwa sare ya mabao 2-2, pamoja na mambo                mengine kuangalia uwezo wa mwanasoka huyo na kuongea nae.
        Mchezaji mwenyewe alipoulizwa                kuhusiana na madai hayo, amejibu kwa kifupi tu akisema,                "Ndio, kuna uwezekano mkubwa wa kucheza Uingereza."
        Vidal alijiunga na Bayern mwezi                Julai mwaka jana kwa dau la pauni mil. 25 na amekuwa                akifanya mambo makubwa katika Ligi Kuu ya Ujerumani,                Bundesliga.
        Manchester United walishindwa                kumsajili Vidal msimu uliopita na kulikuwa na fununu                kwamba bosi mmoja katika klabu hiyo hakupendezwa na                mwanasoka huyo kutoka Chile.
        Alipoulizwa kuhusu skendo hiyo,                mchezaji huyo amesema kuwa ni kweli kulikuwa na fursa ya                kujiunga Man United lakini kuna mambo yalishindikana                katika dakika za lala salama.
        "Nilipenda ofa yao ya kwenda                kujiunga na Man United lakini katika kutafuta mahali                salama na pazuri zaidi kwangu, niliamua kuja Bayern.                Nafikiri uamuzi wangu ulikuwa sahihi kabisa, ingawaje sasa                naona kuna haja ya kupanua wigo zaidi kiuchezaji kwenda                London," amesema.
        
Comments
Post a Comment