"BIASHARA imeisha". Ndivyo            ilivyothibitisha klabu ya Lazio ya Italia kwamba Manchester            United imekubali dili la kumsajili kiungo mshambuliaji wake            Felipe Anderson kwa dau la pauni milioni 46.8.
        Anderson mwenye umri wa miaka 22,            alihusishwa kwa kiasi kikubwa na uhamisho kwenda United katika            dirisha la usajili wa mwezi Januari, ambapo timu hiyo ilisema            kuwa ilipeleka mara mbili maombi ya kutaka huduma yake.
        Mipango hiyo hata hivyo iliharabika baada            ya Lazio kugoma kumuuza, lakini sasa miamba hiyo ya Italia            imesema tayari imemalizana biashara na United.
         "Felipe Anderson atahamia            Manchester United msimu ujao kwa euro milioni 60," alisema            Rais wa Lazio, Claudio Lotito akiwaambia waandishi wa habari            baada ya kuhudhuria mechi ya Serie B wikiendi iliyopita.
        
Comments
Post a Comment