STAA wa zamanai wa Manchester              United, David Beckham amesema kuwa ana matumaini kocha wa              zamani wa Chelsea, Jose Mourinho hivi karibuni atakabidhiwa              kibarua cha kuinoa timu mojawapo ya Ligi Kuu England.        
Mourinho yupo nje ya kazi tangu                alipofukuzwa na Chelsea Desemba mwaka jana, lakini amekuwa                akihusishwa na klabu ya zamani ya Beckham, Manchester                United ambayo inasuasua ikiwa chini ya kocha Louis Van                Gaal.
        Kutokana na hali hiyo, nahodha                huyo wa timu ya taifa ya England amesema kwamba angefurahi                kuona Mreno huyo akirejea katika soka la England mapema                iwezekanavyo.
        "Nina matumaini Mourihno                atarejea kwenye michuano ya Ligi Kuu England hivi                karibuni," Beckham aliuambia mtandao wa TalkSPORT.                "Tunataka makocha wenye uwezo kama huo katika soka letu."              
        
Comments
Post a Comment