BARCLEONA YAFANYA KILICHOTARAJIWA, YAICHAPA ARSENAL 2-0 ...Messi avunja mwiko wa Petr Cech


BARCLEONA YAFANYA KILICHOTARAJIWA, YAICHAPA ARSENAL 2-0 ...Messi avunja mwiko wa Petr Cech

ARSENAL imepata hasara ya kuutumia vibaya uwanja wake wa nyumbani kwa kukubali kichapo cha bao 2-0 kutoka kwa Barcelona katika mchezo mkali wa Champions League.

Vijana wa Arsene Wenger sasa watakuwa na mlima mrefu wa kupanda Nou Camp ambapo ili watinge robo fainali, watahitaji ushindi wa 3-0.

Lionel Messi alikuwa mwiba kwa Arsenal kwa kufunga mabao yote mawili, la kwanza likija dakika ya 71 na la pili likiwasili kwa njia ya penalti kunako dakika ya 83.

Hii ni mara ya kwanza kwa Lionel Messi kumtungua kipa Petr Cech na ni mara ya kwanza kufunga ugenini dhidi ya timu za England.

Kimahesabu safari ya Arsenal kwa mara nyingine tena inakomea hatua ya 16 bora kwa mwaka wa sita mfululizo.

Katika miaka mitano iliyopita, Arsenal ilijikuta ikipoteza mchezo wa kwanza hatua ya 16 bora kwa zaidi ya goli moja. Ilipoteza 4-0 kwa AC Milan, 3-1 na 2-0 kwa Bayern Munich kabla ya kufungwa 3-1 na Monaco.

Arsenal (4-2-3-1): Cech 7, Bellerin 6.5, Mertesacker 5.5, Koscielny 6, Monreal 7, Coquelin 7 (Flamini, 81, 4), Ramsey 7.5, Oxlade-Chamberlain 5.5 (Walcott, 50, 6), Ozil 6, Sanchez 7 Giroud 5.5 (Welbeck, 73, 6.5)

Barcelona (4-3-3): Ter Stegen 7, Alves 7, Pique 6.5, Mascherano 6.5, Alba 6, Rakitic 6, Busquets 7, Iniesta 7, Messi 8, Suarez 6.5, Neymar 7.

The away side's brilliant front three were all                  involved as Messi calmly slotted the ball past Petr                  Cech
 Messi akipiga mpira unaompita kipa Petr Cech na kuwa bao la kwanza kwa Barcelona
Argentinian showed his                    nerve from the spot to double the lead and put                    Barcelona on the brink of qualification
Messi akifunga bao la pili kwa mkwaju wa penalti
Barcelona's No 9 Luis                    Suarez holds his face in disbelief after missing a                    golden chance at the Emirates
Namba 9 wa Barcelona Luis Suarez akisikitika baada ya kukosa bao la wazi









Comments