BARCELONA KUWEKA MEZANI PAUNI MIL 23 ILI KUMNASA RIYAD MAHREZ WA LEICESTER CITY



BARCELONA KUWEKA MEZANI PAUNI MIL 23 ILI KUMNASA RIYAD MAHREZ WA LEICESTER CITY
Riyad Mahrez's            sensational form has helped Leicester towards qualification            for the Champions League
 BARCELONA inapanga kuizidi kete Chelsea kwa kumsajili winga wa kimataifa wa Algeria anayekipiga Leicester City, Riyad Mahrez kwa dau la pauni milioni 23.

Mwarabu huyo mwenye umri wa miaka 25, amekuwa na kiwango cha juu akiwa na vinara hao wa Premier League aliowafungia mabao 15 na kupika mengine 10 msimu huu.

Gazeti la Daily Star limesema kuwa Chelsea inaangalia uwezekano wa kunasa saini ya winga huyo ambaye anatajwa kumvutia mmiliki wa klabu hiyo, Roman Abramovich, lakini sasa rpoti kutoka Hispania zinapasha kwamba Barcelona nayo imejitosa katika dili hilo na kuachana na mipango ya kumtwaa mshambuliaji wa Celta Vigo, Nolito.

Barca ilipeleka maombi mara kadhaa kwa ajili ya mshambuliaji huyo Mhispania bila mafanikio, na sasa imeamua kugeuzia mipango yake kwa Mahrez ambaye kasi yake na maamuzi ya haraka vimemshawishi Luis Enrique kwamba anafiti katika safu yake ya mashambulizi.

Mahrez alitua England mwaka 2014 akiwa si mchezaji wa kujulikana, akitoka kuitumikia kwa miaka mine klabu ya Le Havre ya Ufaransa.


Comments