BARCELONA HAWASHIKIKI, SUAREZ HAZUILIKI ...Las Palmas yapigwa 2-1



BARCELONA HAWASHIKIKI, SUAREZ HAZUILIKI ...Las Palmas yapigwa 2-1
Luis Suarez na Neymar wamefunga kwa mara nyingine tena na kuiongoza  Barcelona kushinda  2-1 kwenye mchezo wa La Liga dhidi ya Las Palmas.

Ushindi huo unafanya Barcelona izidi kutanua rekodi yake hadi kufikia mechi 32 bila kupoteza mchezo.

Suarez alifunga katika dakika ya sita tu huku Neymar akifunga kabla ya mapumziko hiyo ikiwa ni baada ya Willian Jose wa Las Palmas  hajafanya matokeo yasomeke 1-1.
Barcelona's Luis Suarez, center, celebrates scoring the              opening goal during a Spanish La Liga soccer match against              Las Palmas, at the Gran Canaria stadium in...
Luis Suarez akipongezwa baada ya kuifungia Barcelona bao la kwanza 



Comments