ARSENE Wenger ana matumaini kuwa rekodi ya            kipa wake Petr Cech dhidi ya Lionel Messi itamnyamazisha staa            huyo wa Barcelona watakapokutana katika mechi ya awali ya Ligi            ya Mabingwa hatua ya 16 bora leo usiku.
        Mshambuliaji huyo raia wa Argentina            hajafanikiwa kumfunga kipa huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya            Czech katika mechi nane zilizopita na Wenger anaamini rekodi            hiyo itamchanganya Messi kiasi cha kushindwa kutekeleza wajibu            wake kisawasawa dimbani.
        Messi amejipambanua kuwa mchezaji bora            zaidi duniani na Cech atahitaji kuwa katika ubora wake kuweza            kumtuliza.
        Wenger anaukubali 'muziki' wa Barcelona            linapokuja suala la mashambulizi na kwamba hajaona machezaji            mwenye rekodi ya kutisha kama Messi, lakini anaamini kuwa            historia iko upande wao dhidi ya staa huyo.
        
Comments
Post a Comment