UONGOZI wa Yanga, umeeleza kwamba wakati wowote unaweza            kuamua kutumbua jipu kama anavyofanya rais wa Jamhuri ya            Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli kwa kuanika            wanaoihujumu.
        Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa            klabu hiyo, Jerry Muro wakati akizungumza na Saluti5 na            kufafanua kuwa wapo mbioni kufanya hivyo kutokana na kuwapo            hali ya kutaka kuzibeba baadhi ya timu.
        Alisema, wamegundua timu hizo zimekuwa zinabebwa na            viongozi ambao wapo ndani ya Shirikisho la Soka nchini (TFF),            ili kuzipa nafasi baadhi ya timu kutokana na wao kupangiwa            kucheza mechi huku timu nyingine zikisubiri.
        "Tunajua wazi kwamba sisi tunapangwa kucheza kwanza            huku wenzetu wanaangalia nini tunafanya bila wao kucheza, hapo            kuna kasoro ukweli tutauweka wazi kama anavyotumbua majipu            rais wetu Magufuli," alisema Muro.
        
Comments
Post a Comment