Hatimaye kocha wa Chelsea Jose              Mourinho ametimuliwa kazi baada ya mwenendo mbovu msimu huu.
        Sasa Roman Abramovich atalazimika              kumlipa Jose Mourinho zaidi ya pauni milioni 40 ikiwa ni              mshahara wake wa sehemu iliyobakia kwenye mkataba wake              uliovunjwa.
        Abramovich, tajiri wa Kirusi              anayemiliki Chelsea, aliongoza kikao cha bodi ya timu akiwa              na menejimenti yake - Bruce Buck, Marina Granovskaia, Eugene              Tenenbaum na Michael Emenalo — ambapo iliamuliwa Mourinho              atimuliwe. 
        Kuunununua              mkataba wake wa miaka minne wenye thamani ya pauni 250,o00              kwa wiki, ni ilikuwa ni moja ya sababu kubwa za kushindwa              kumtimua Mourinho mapema, mara tu baada ya kusaini mkataba              huo mpya.
        Mourinho              alikubabali kusaini mkataba mpya mwishoni mwa mismu uliopita              na ilipofika mwezi Agust klabu ikatangaza rasmi mkataba huo              wa miaka minne wa kocha huyo wa Kireno.
        Baada              ya kushinda taji la Premier League kiulaini msimu uliopita,              Chelsea ikaamini kuwa Mourinho ni kocha bora duniani na              ikampa moja kwa moja mkataba mpya wa miaka minne bila kuweka              kipengele cha manunuzi ya mkataba huo iwapo klabu hiyo              ingeamua kumtimua.
        Mwaka 2007            Septemba, alimlipa Mourinho na benchi lake la ufundi pauni            milioni 16 pale alipomtimua ingawa baadae alimtumia kocha huyo            gari la kifahari aina ya Ferrari kama shukrani kwa kazi yake            aliyoifanya Chelsea.
        
Comments
Post a Comment