Alexis Sanchez            amepata kikwazo cha kurejea uwanjani wakati akielekea kupona            maumivu yake ya msuli wa paja na sasa kocha wa Arsenal, Arsene            Wenger amesema nyota huyo atarejea kikosini mwezi Januari. 
        Mshambuliaji huyo            ambaye aliumia katika mchezo wa sare ya 1-1 dhidi ya Norwich            mwezi uliopita, alitarajiwa kuwa kwenye kikosi cha Arsenal            kilichoichapa Manchester City 2-1 Jumatatu usiku, lakini sasa            mambo yamwekwenda kombo kwake.
        Baada ya mchezo huo            wa Premier League dhidi ya City, Wemger alisema: "Nadhani            Sanchez atarejea uwanjani Januari 10. Amepata vikwazo kidogo            siku mbili zilizopita. Tulitarajia angekuwa kwenye benchi leo            (jana) usiku".
        Alexis                Sanchez (pichani katikati) akifuatilia mchezo wa Arsenal                na Manchester City
        Sanchez              aliumia msuli wa paja katika mechi ya  forward 1-1 dhidi ya Norwich                mwezi uliopita
        Wenger                alikuwa na matumaini kuwa  Sanchez angecheza dhidi ya Man                City Jumatatu usiku lakini sasa mshambuliaji huyo atarejea                uwanjani mwezi Januari
          Sanchez                ameichezea Arsenal mechi 20 msimu huu na kufunga magoli 9
        
Comments
Post a Comment