Wayne Rooney ambaye hajasafiri na kikosi cha Manchester United kwenda Ujerumani, Jumatatu usiku alijitosa kwenye uwanja wa Goodison Park kwenda kushuhudia mchezo wa Ligi Kuu baina ya timu yake ya zamani Everton na Crystal Palace.
Rooney hakuwa peke yake bali aliandamana na mwanae Kai ambapo walionekana na tabasamu pana wakati mchezo huo wa sare ya 1-1 ukiendelea.
Nahodha huyo wa United alifunga dhidi ya Everton mwezi Oktoba kwenye uwanja huo huo wa Goodison Park wakati kikosi cha Van Gaal kilipozoa ushindi wa bao 3-0.
Wayne Rooney akiwa ndani ya Goodison Park Jumatatu usiku kushuhudia mechi ya Everton na Crystal Palace
Rooney akiwa uwanjani na mwanae
Roy Keane pia alikuwepo uwanjani
Comments
Post a Comment