WAKALA wa mchezaji mahiri wa timu              ya soka ya Manchenster United ya nchini Uingereza, Wayne              Rooney, amesema kwamba mchezaji huyo hana mpango wa kutaka              kutua nchini China kama inavyoripotiwa.
        Taarifa iliyotolewa na wakala              huyo, imeeleza kwamba mchezaji huyo hajawahi kukutana na              viongozi wa timu yoyote ya nchini humo na kueleza kwamba              bado ana mkataba wa kuitumikia Manchester United.
        Aliema yeye kama msimamizi wa              mchezaji huyo, hana taarifa yoyote ya mkali huyo kutakiwa              nchini China kama inavyoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya              habari.
        Majuzi              iliripotiwa kuwa klabu ya Shanghai SIPG              inayonolewa na kocha za zamani wa England Sven              Goran Eriksson imetenga pauni milioni 75 ili kumnasa Rooney.
        Katika habari hizo, ikadaiwa kuwa              klabu hiyo ipo tayari kumpa Rooney mkataba wa miaka mitatu              wenye thamani ya pauni milioni 25 kwa msimu.
        Rooney              kuungana tena na Sven Goran Eriksson?
        
Comments
Post a Comment