KLABU ya Manchester United imeendelea kufanya vibaya            katika Ligi Kuu ya England, lakini kocha wake Louis Van Gaal            anasema hawatakata tamaa.
        Kocha huyo raia wa Uholanzi aliyasema hayo baada ya            juzi kupigwa mabao 2-1 na timu ya Bournemouth.
        Kipigo hicho kimewafanya United waendelee kuganda            nafasi ya nne katika msimamo lakini wakiwa pointi nne tu nyuma            ya vinara wa Ligi hiyo, Arsenal.
        "Inaumiza na kuvunja moyo kupoteza mechi mbili            mfululizo lakini hatutakata tamaa ya ubingwa kwasababu            kimsimamo bado hatujashuka sana, ni suala la kujipanga na            kupambana kwa nguvu zaidi," aisema Van Gaal.
        Aliema atahakikisha kikosi hicho hakiruhusu tena            kupoteza mchezo wowote katika kipindi hiki cha mechi nyingi za            sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya, ambacho ndicho huwa kigumu            kwa kila timu.
        Louis Van Gaal amewahakikishia mashabiki wa klabu hiyo            kuwa, hawatatoka mikono mitupu msimu huu.
        
Comments
Post a Comment