WAKATI klabu kadhaa zikionekana kummezea mate Luis            Suarez FC Barcelona, mpiga mabao huyo amesema kwamba ana            furaha isiyo kifani kuwa hapo kuliko kwenye timu nyingine            yoyote barani Ulaya.
        Suarez amesema hafikirii kuondoka Barcelona kwa vile            hiyo ni klabu kubwa duniani lakini pia La Liga ndiyo ligi bora            kuliko zingine zote.
        Alieleza kwamba miongoni mwa vitu ambavyo vimekuwa            vinamfanya aipende La Liga, ni ushindani kuanzia kwa wachezaji            hadi timu sambamba na hamasa za mashabiki. 
        "Mashabiki wamekuwa chachu ya mafanikio yangu ndani ya            uwanja, sio siri kwamba nikiendelea kuwapo ndani ya timu hii            nitapata mafanikio makubwa," alisema nyota huyo ambaye alitua            Barca akitokea timu ya Liverpool ya Uingereza na kuongeza:            "Unaanzaje kufikiria kuondoka Barcelona?"
        Majuzi Suarez alipata tuzo ya              dhahabu baada ya kuwa mfungaji bora wa Klabu Bingwa ya Dunia              na kuisaidia Barcelona kutwaa taji hilo mbele ya River Plate              ya Argentina.
        
Comments
Post a Comment