KOCHA mpya wa klabu ya Valencia ya Hispania, Gary            Neville (pichani juu), amemwagiwa sifa na kocha wa zamani wa            Manchester United, Sir Alex Furguson kuwa ni mwenye bahati            katika medani hiyo.
        Neville alianza kazi ya kuinoa Valencia mwanzoni mwa            juma hili baada ya mechi ya sare ya 1-1 na Barcelona,            akishuhudiwa na mamia ya mashabiki wa klabu hiyo.
        Akizungumza katika mkutano wa Tech Crunch Disrupt,            jijini London, Fergie alisema kila anachogusa Gary Neville hubadilika na kuwa dhahabu.
        Fergie alisema, Neville amekuwa mtu ambaye inakuwa            vigumu kuamini anachokifanya kwani amekuwa akifanya vizuri            katika kila sekta.
        Aidha, Fergie alisema hata alipokuwa kwenye uchambuzi            katika luninga, amekuwa wa kustaajabisha na kwamba hata sasa            katika klabu hiyo ya Valencia atapata mafanikio.
        Neville alitoa maisha yake kwa kocha Fergie kwa miaka            19 akitwaa mataji mengi na akiitumikia timu ya taifa mechi 85.
        
Comments
Post a Comment