RONALDO APIGA MBILI REAL MADRID IKIUA 3-1 KWA REAL SOCIEDAD



RONALDO APIGA MBILI REAL MADRID IKIUA 3-1 KWA REAL SOCIEDAD
Nacho            (centre) and Benzema (right) desperately jump to carve a            chance at the Sociedad goal, but the away side clear their            lines

Hata anapokuwa kwenye fomu mbovu bado ni hatari, Cristiano Ronaldo alikosa penalti kipindi cha kwanza lakini bado akafunga mabao wawili yaliyoiwezesha Real Madrid kuinyuka Real Sociedad 3-1 na kumpa ahueni kocha aliyekalia kiti cha moto Rafa Benitez.

Muda mfupi kabla mchezo haujaanza, mashabiki waliojazana uwanjani walikuwa wakipiga makelele ya kumkandia kocha Benitez huku pia baadhi ya wachezaji wakionekana wazi kucheza chini ya kiwango chao ili kumkomoa.

Ilionekana kama vile Ronaldo amejiunga na kundi hilo la wachezaji baada ya kupaisha penalti yake lakini muda mfupi baadae akapata penalti nyingine na kuujaza mpira wavuni hiyo ikiwa ni dakika tatu kabla ya mapumziko.

Real Sociedad walisawazisha dakika ya 49 kupitia kwa Bruma kabla Ronaldo haijafungia Real Madrid bao la pili dakika ya 67 huku Lucas Vazquez aliyetokea benchi akihitimisha ushindi kwa goli la dakika ya 86.

Real Madrid XI: Navas, Danilo, Pepe, Nacho, Marcelo, Kroos, Modric (Casemiro 87), James (Kovacic 59), Ronaldo, Benzema (Lucas Vazquez 75), Bale

Real Sociedad XI: Rulli, Martinez, Aritz Elustondo, Inigo Martinez, Yuri, Markel, Illarramendi, Prieto, Canales (Pardo 45), Agirretxe (Bruma 18), Jonathas (Vela 68)

Cristiano Ronaldo tucks away                  a penalty - his second spot-kick of the match - to give                  Real Madrid the lead against Real Sociedad
Cristiano Ronaldo anafunga kwa penalti
Ronaldo runs towards the                  home fans at the Bernabeu Stadium to celebrate giving                  Real Madrid the lead in their final match of the year
Ronaldo akikimbia kwenda kushangilia mbele ya mashabiki Bernabeu Stadium 
Ronaldo (centre) celebrates                  alongside Real Madrid team-mates Gareth Bale (left),                  Marcelo (right) and Karim Benzema after making it 1-0
Ronaldo (katikati) akishangilia na wachezaji wenzake wa Real Madrid  Gareth Bale (kushoto), Marcelo (kulia) na Karim Benzema baada ya bao la kwanza
Ronaldo (right) celebrates                  after scoring his second penalty of the match to make up                  for his first, which was blazed over the crossbar
Ronaldo (kulia) akishangilia bao lake la penalti
Ronaldo produces his                  trademark celebration after slotting his penalty home to                  give Real Madrid the lead against Real Sociedad
Ronaldo na mbwembwe zake za ushangiliaji
Young Portuguese talent Bruma produced a wonder                  curled finish to level the scores just after half-time                  at the Bernabeu Stadium
Kinda hatari wa Ureno Bruma akishangilia bao pekee la Real Sociedad



Comments