ROMAN ABRAMOVICH ASEMA PEP GUARDIOLA LAZIMA ATUE CHELSEA …amwandalia mshahara mnono, fungu kubwa la usajili, Guardiola asema Chelsea inahitaji wachezaji 10 wapya
Chelsea inatarajia            kuwa maisha ya London yatakuwa kivutio cha wao kumnyakua kocha            wa Bayern Munich Pep Guardiola            mbele ya Manchester City.
        Mabingwa hao            watetezi wa Premier League wanaandaa ofa nono ili kuipiku            Manchester City ambayo ilikuwa imekaa sehemu nzuri kupata            huduma ya kocha huyo bingwa wa soka la 'draft'.
        Tajiri wa Chelsea            Roman Abramovich amekataa kukata tamaa ya kumnasa Guardiola -            ambaye aliikwepa Chelsea mwaka 2012. 
        Daily Mail            la Uingereza limefichua kuwa Abramovich            amedhamiria kumfanya kocha huyo awe kocha anayelipwa pesa            nyingi duniani kuliko kocha mwingine yeyote yule, ikiwa ni            pamoja na kumpa fungu nono la kukifumua kikosi chake.
        Chelsea                inaamini inampeleka Pep Guardiola Stamford Bridge
        Guardiola                amethibitisha kuwa anaondoka Bayern mwishoni mwa msimu huu
        Tajiri                wa Chelsea  Roman Abramovich atampa Guardiola fungu la                kukifumua kikosi 
          Chelsea inaamini mke wa  Guardiola, Cristina                  (kulia), anapendelea zaidi maisha ya London 
            Abramovich              alikuwa akimlipa  Jose Mourinho              pauni 250,000 kwa wiki (pauni milioni 12 kwa mwaka) kabla              hajaamua kumtimua Alhamisi iliyopita.
          Daily Maily linaadikia pia              kuwa Guardiola ameshakifanyia tathmini kikosi cha Chelsea na              kusema kuwa klabu hiyo itahitaji kusajili wachezaji 10 wapya              msimu ujao.
          
Comments
Post a Comment