REAL MADRID YAFANYA MAUAJI, YAPIGA MTU 8-0 …Ronaldo afunga 4 na kuweka rekodi mpya, Paris Saint Germain nayo yashinda



REAL MADRID YAFANYA MAUAJI, YAPIGA MTU 8-0 …Ronaldo afunga 4 na kuweka rekodi mpya, Paris Saint Germain nayo yashinda


Cristiano Ronaldo ameweka rekodi mpya hatua ya makundi Champions League wakati Real Madrid ikiichapa Malmo bao 8-0.

Ronaldo akafunga mara nne na kufanikiwa kujikusanyia jumla ya mabao 11 hatua ya makundi ambayo ni rekodi mpya kwenye michuano hiyo.

Karim Benzema naye akafunga mara tatu huku bao lingine la Real Madrid likifungwa na Mateo Kovacic.


Hata kabla ya mchezo huo, Real Madrid ilishajihakikishia nafasi ya kwanza kwenye kundi A, lakini hiyo haikuwa sababu ya kuacha kuingushia Malmo kipigo cha mbwa mwizi.


Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Paris Saint Germain iliyoshika nafasi ya pili, ikaichapa Shakhtar Donetsk 2 – 0 kwa magoli ya Lucas Moura na Zlatan Ibrahimovic.
The 2-year-old thanks his                    team-mate who provided the chances for both of his                    first-half goals with some excellent wing playWachezaji wa Real Madrid wakipongezana
Ronaldo was on the                      scoresheet himself six minutes before the break,                      firing in a free kick from wide on the left hand                      side to make it 3-0 
Ronaldo akifunga moja ya mabao yake manne
It was a night to remember                    for the Portuguese forward, who had things all his own                    way against a weak Malmo side
Ronaldo akishangilia bao lake la tatu





Comments