RAFA BENITEZ ASEMA LAZIMA ASAJILI MSAIDIZI WA RONALDO NA BENZEMA



RAFA BENITEZ ASEMA LAZIMA ASAJILI MSAIDIZI WA RONALDO NA BENZEMA
Gareth Bale will be            keen to turn around his much-criticised form after La Liga's            fifth-placed side
KOCHA mkuu wa timu ya Real Madrid ya Hispania, Rafa Benitez, ametamba kuwa bado anapenda kusajili mchezaji mmoja mwenye kasi ya kukimbia ili aweze kupata mabao zaidi.

Benitez amesema amekuwa akipata wakati mgumu kutokana na kukosa mtu mwenye mbio za kushitukiza wa kusaidiana na Cristiano Ronaldo na Karim Benzema.

"Yapo baadhi ya mambo kwa upande wangu ni magumu, hasa kipindi cha usajili cha dirisha dogo, nimepanga kusajili mshambuliaji lakini nina kila sababu ya kujipanga ili kumnasa nyota ambaye ana msaada mkubwa ndani ya dimba," alisema kocha huyo.

Hata hivyo, Benzema alisema kwamba bado anaendelea na kazi hiyo kwa usiri mkubwa asije akavurugiwa na baadhi ya makocha wa timu nyingine.


Comments