KOCHA wa Real Madrid, Rafa Benitez amesema  ana imani            kubwa ya kumnasa mshambuliaji wa  Bayern Munich, Robert            Lewandowski katika msimu ujao.
        Benetez alisema kuwa amekuwa akivutiwa na uwezo mkubwa            wa mchezaji huyo kwa namna anavyoweza kuwahadaa mabeki na            ubora wake wa kuwachambua magolikipa hata pale anapokuwa na            nafasi finyu.
        Habari za ndani kutoka Madrid zinadai kuwa timu hiyo            tayari imeanza mikakati ya kimya kimya kuhakikisha inamnasa            staa huyo wa Poland  licha ya kuwepo ushindani kutoka kwa timu            kadhaa  barani Ulaya.
        "Huyu ni mchezaji mzuri, lakini anaweza kuwa mkali            zaidi  akija hapa Madrid, kazi hiyo imeanza kufanyika kwa            mafanikio makubwa," kilisema chanzo kimoja cha Real Madrid.
        
Comments
Post a Comment