WACHEZAJI wa Arsenal wakiongozwa na kipa mkongwe, Petr            Cech, wamejitapa kwamba msimu huu watatwaa ubingwa wa Ligi Kuu            England.
        Jeuri hiyo ya Arsenal imekuja baada ya klabu hiyo            kufanikiwa kumaliza nusu ya msimu huku ikiwa kileleni mwa Ligi            Kuu.
         "Ukiangalia            tangu kuanza kwa msimu huu, tumepoteza michezo minne tu hadi            kufikia mwisho wa Disemba, sio kazi rahisi, nadhani tunaweza            kuhitimisha vizuri," alisema Petr Cech aliyeweka rekodi mpya            England ya kuwa akipa aliyecheza mechi nyingi bila kufungwa            (clean sheet).
        Cech mwenye miaka 33, ambaye ni kipa aliyeipa mafanikio            makubwa Chelsea kabla ya kutupiwa virago mwishoni mwa msimu            uliopita, alisema wachezaji watapigania ushindi kila mechi.
        Aliongeza kusema kuwa, ikiwa wameweza kuituliza            Manchester City, haoni ni kwanini washindwe kuzifunga timu            nyingine. 
        Arsenal haijawahi kutwaa taji la Ligi Kuu tangu msimu            wa 2003-04 ilipoandika historia ya kutopoteza mchezo hata            mmoja.
        Hata hivyo, kocha wa Arsenal amelia kuwakosa wachezaji            kadha muhimu wa kikosi chake kutokana na kuwa majeruhi,            wakiwemo Jack Wilshere, Francis Coquelin, Danny welbeck, Sant            Cazorla na Tomas Rosicky.
        
Comments
Post a Comment