OLIVIER GIROUD AIPELEKA ARSENAL 18 BORA YA CHAMPIONS LEAGUE … Olympiacos yalala 3-0 kwa vijana wa Wenger, Bayern Munich yaendeleza kichapo


OLIVIER GIROUD AIPELEKA ARSENAL 18 BORA YA CHAMPIONS LEAGUE … Olympiacos yalala 3-0 kwa vijana wa Wenger, Bayern Munich yaendeleza kichapo
Olivier Giroud was the            hero for Arsenal as he scored a hat-trick to see them past            Olympiacos and into the knockout stages
Hatimaye Arsenal imepangua wingu zito lililokuwa limetanda mbele yao kwenye hatua ya makundi ya Champions League na kuichabanga Olympiacos 3-0 kwenye mchezo wa kundi F.

Ushindi huo umetosha kabisa kuivusha Arsenal kwenda hatua ya 16 bora ikiwa ni mwaka wa 16 mfululizo kutinga hatua hiyo.

Shujaa wa Arsenal alikuwa ni mshambuliaji Olivier Giroud aliyefunga mabao yote matatu katika dakika ya 29 na 49 huku bao lake la tatu akifunga dakika ya 67 kupitia mkwaju wa penalti.

Arsenal ambao walikubali kichapo cha bao 3-2 kutoka kwa Olympiacos walipocheza kwenye dimba lao la Emirates, Jumatano hii wakiwa ugenini kwenye uwanja wa Georgios Karaiskakis jijini Athens, Ugiriki, wakacharuka na kufanya kile kilichohitajika.

Ili kusonga mbele kwa tofauti ya mabao, Arsenal ilitakiwa ishinde kwa zaidi ya bao moja ili kuipiku Olympiakos.

Katika mchezo mwingine wa kundi F, Bayern Munich imeendeleza ubabe kwa kuichapa Dinamo Zagreb 2-0 mabao yote yakifungwa na Robert Lewandowski katika dakika ya 61 na 64.

Olympiacos: Roberto 4, Elabdellaoui 5, Da Costa 5, Siovas 5, Masuaku 5, Kasami 5 (Dominguez 71, 5), Milivojevic 5, Seba 5 (Hernani 77, 5), Fortounis 6.5, Pardo 5 (Finnbogason 86), Ideye 5.

Arsenal: Cech 7, Bellerin 6.5, Mertesacker 7.5, Koscielny 7.5, Monreal 7, Ramsey 7.5, Flamini 7, Walcott 7 (Gibbs 72, 6), Ozil 9, Campbell 8.5 (Oxlade-Chamberlain 90), Giroud 9.5 (Chambers 90).
Olivier Giroud was the hero                  for Arsenal as he scored a hat-trick to see them past                  Olympiacos and into the knockout stages
Olivier Giroud amekuwa shujaa wa  Arsenal kwa kufunga magoli yote matatu dhidi ya  Olympiacos na kutinga hatua ya mtoano
The Frenchman scored all                  three goals as Arsenal rescued their Champions League                  hopes with a vital victory in Athens on Wednesday
Olivier Giroud akishangilia na wenzake
Giroud celebrates his                  hat-trick with team-mate Theo Walcott after helping                  Arsenal secure progress in the Champions League
Giroud akishangilia hat-trick yake 
Msimamo wa kundi F baada ya kukamilika kwa mechi zote






Comments