MOURINHO ASEMA SULUHISHO LA DIEGO COSTA NI KUMNUNUA ANTOINE GRIEZMANN



MOURINHO ASEMA SULUHISHO LA DIEGO COSTA NI KUMNUNUA ANTOINE GRIEZMANN
Chelsea manager Jose            Mourinho believes owner Roman Abramovich still has faith in            him .
HATIMAYE kocha Jose Mourinho amekubali kuwa Chelsea inaangushwa na kukosekana kwa mshambuliaji mwenye uwezo wa kupiga mabao.

Amesema, uwezo wa Diego Costa umeshuka hivyo yupo tayari kumnunua mshambuliaji wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann katika usajili wa Januari.

"Kwa kweli hatuna namna ni lazima tufanye usajili wa washambuliaji wawili au watatu katika mwezi Januari," alisema Joe Mourinho.

Kocha huyo alikiri kuwa majeruhi kwa Loic Remy na Radamel Falcao kunamlazimisha kuwatumia viungo katika nafasi ya ushambuliaji.

Chelsea Jumamosi ilipigwa mweleka na timu ya Bournemouth hivyo kuzidi kusota kwenye nafasi ya 14 ikiwa na pointi 15.

Gazeti la The Mirror limefichua kuwa Atletico iko tayari kumwachia staa wake huyo kama itawekewa mezani paundi mil. 25 pamoja na mchezaji mmoja.

Imefichuliwa kuwa kukosa mshambuliaji mwingine na matokeo kuzidi kuwa mabaya kunamlazimisha Mourinho kumpanga Costa licha ya kuwa na bifu nae.


Comments