MCHEZAJI Breel Embolo anayekipiga FC Basel ya nchini            kwao Uswisi, amepigiwa debe kwamba ndio chaguo kubwa la kocha            Louis Van Gaal.
        Taarifa iliyotolewa na vyombo vyahabari nchini humo,            imeeleza kwamba mchezaji huyo huenda akatua katika timu ya            Manchester United katika usajili wa dirisha dogo.
        Mkali huyo ameanza kufuatiliwa na timu hiyo ili kuondoa            kasoro kwenye safu ya ushambuliaji ya timu hiyo inayoshiriki            Ligi Kuu nchini Uingereza.
        Hata hivyo, hadi juzi, United imeshindwa kutaja dau            ambalo wamelitenga kwa ajili ya kutaka kumsajili mkali huyo.
        
Comments
Post a Comment