Mashujaa Band imefumua safu ya uongozi kwa upande wa            wanamuziki na kukifutilia mbali cheo cha rais wa bendi.
        Nafasi ya rais wa bendi iliyokuwa ikishikiliwa na            mwimbaji 'ghali' wa dansi, Chaz Baba, imeondolewa na badala            yake sasa kutakuwa na kiongozi wa bendi.
        Chaz Baba sasa anakuwa mwanamuziki wa kawaida huku            kiongozi wa muda wa bendi akiwa rapa Ferguson.
        Mkurugenzi wa Masoko wa Mashujaa, Maxi Luhanga            ameithibitishia Saluti5 juu ya mabadiliko hayo na kusema hiyo            ni hatua ya mpito hadi hapo wanamuziki watakapofanya uchaguzi            kuchagua uongozi mpya.
        Akiongea na Saluti5, Chaz Baba aliyevuliwa urais,            akasema amefurahishwa na hatua hiyo na anafurahi kuwa            mwanamuziki wa kawaida.
        "Uongozi ni mzigo na sijambo baya kupokezana mzigo huo,            nimefurahia sana mabadiliko hayo, sina kinyogo," alisema Chaz            Baba.
        
Comments
Post a Comment