TETESI zinadokeza kuwa, kocha wa zamani wa Manchester            United, Sir Alex Ferguson ametakiwa kumpiga tafu Louis Van            Gaal.
        Imeelezwa kuwa, mabosi wa klabu hiyo ya Old Trafford            wametishwa na mwenendo wa timu hiyo na wanahofia kumfukuza            kazi kocha wao ili kutotibua zaidi mambo.
        Imedaiwa kuwa Ferguson aliketi na Makamu Mwenyekiti wa            United, Ed Woodward na Mtendaji Mkuu wa zamani wa klabu iyo,            David Gill hapo Old Trafford mwishoni mwa wiki.
        Ferguson kocha aliyeipa timu hiyo mafanikio yasiyo            kifani katika miaka 27 aliyoiongoza, hajasema lolote kuhusu            tetesi hizo za kutakiwa umsaidia Van Gaal.
        
Comments
Post a Comment