Safari ya Manchester United katika kusaka mafanikio            kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu huu, imefikia            kikomo baada ya kufungwa 3-2 na Wolfsburg ya Ujerumani.
        Kwa matokeo hayo, United imeshika nafasi ya tatu kundi            B baada ya PSV kuinyuka CSKA Moscow 2-1 katika mchezo mwingine            wa kundi hilo.
        Wolfsburg inayoongoza kundi B, inasonga mbele kwenye 16            bora sambamba na PSV iliyoshika nafasi ya pili.
        Ili kusonga mbele, United ilihitaji kushinda mchezo            huo, lakini mambo yamekwenda kombo licha ya kuongoza kwa bao            la mapema kupitia kwa Anthony Martial kunako dakika ya 10.
        Wolfsburg ikaenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 2-1            kufuatia mabao ya Naldo dakika ya 13 na Vieirinha dakika ya            29.
        United ikasawazisha dakika ya 82 kwa bao la kujifunga            la Joshua Guilavogui lakini Naldo akaifungia Wolfsburg bao la            ushindi dakika mbili baadae.
        
Comments
Post a Comment