MANCHESTER UNITED NA TOTTENHAM ZAWANIA SAINI YA RIYAD MAHREZ WA LEICESTER CITY


MANCHESTER UNITED NA TOTTENHAM ZAWANIA SAINI YA RIYAD MAHREZ WA LEICESTER CITY

Winga wa Leicester Riyad Mahrez amekuwa bidhaa adimu baada ya Tottenham nayo kuhusishwa na usajili wa nyota huyo wa kimataifa wa Algeria.

Manchester United imekuwa klabu ya kwanza kuhusishwa na Mahrez ambaye ameifungia  Leicester mabao 14 msimu huu.

Klabu zote hizo mbili zinatajwa kuwania saini ya Mahrez katika usajili wa dirisha dogo la Januari ingawa Leicester imeshapiga mkwara kuwa haitauza mchezaji yoyote katikati ya msimu.

Leicester inaongoza Premier League kwa pointi 38 na katika hali ya kawaida, haitarajiwi kuingia kwenye mipango ya kubomoa timu kwa kuuza nyota wake hali itakayoodhohofisha mbio zao za kusaka taji la Ligi Kuu.

Manchester United and                  Tottenham are both interested in Leicester's red hot                  winger Riyad Mahrez
Manchester United na Tottenham wanapigana vikumbo kwa Riyad Mahrez
Mahrez scored his 13th and                  14th Premier League goals from the penalty spot against                  Everton on Saturday
Mahrez alifunga goli lake la 13 na 14  kwa njia ya penalti dhidi ya Everton Jumamosi iliyopita


Comments