MANCHESTER UNITED NA KIWEWE CHA USAJILI ...SASA WATAJWA KUMWANIA GARETH BALE DIRISHA DOGO LA JANUARI


MANCHESTER UNITED NA KIWEWE CHA USAJILI ...SASA WATAJWA KUMWANIA GARETH BALE DIRISHA DOGO LA JANUARI
England will face            Gareth Bale (pictured) and Co in the group stage at Euro 2016            next summer 
MANCHESTER United imehusishwa na usajili ulio sawa na njozi za mchana za kumnasa straika wa Real Madrid, Gareth Bale katika dirisha dogo la Januari.

Mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham ametajwa katika orodha ya usajili wa kocha wa Maashetani hao, Louis Van Gaal ambaye anapambana kuokoa kibarua chake.

Hata hivyo tayari Real Madrid imekanusha juu ya Bale kuhamia United ambayo katika siku za hivi karibuni imekuwa ikihusishwa na usajili wa wachezaji kadhaa wa kadha.

Mbali Bale, pia United imekuwa ikihusishwa kutaka kumrejesha kikosini straika wake wa zamani, Cristiano Ronaldo.

Hata hivyo, mara kadhaa Ronaldo amekuwa akizungumzia suala la yeye kurejea Old Trafford kuwa ni jambo linalowezekana, ila linahitaji subira ya kipindi kirefu kijacho.

Taarifa za usajili za hivi karibuni zinasema, Bale amekuwa chaguo la kwanza katika orodha ya usajili wa Old Trafford huku ikidaiwa kuwa  Van Gaal anahitaji mchango wa mwanandinga huyo aliyetua Madrid kwa dau nono la pauni mil. 80.

Tayari Man United imeweka mezani kitita cha pauni mil. 60 kwa aili ya kumnasa Bale, huku kukiwa na tarifa za kutaka kuongeza dau zaidi.


Comments