MANCHESTER UNITED NA KIWEWE CHA USAJILI ...SASA WATAJWA KUMWANIA GARETH BALE DIRISHA DOGO LA JANUARI
MANCHESTER United imehusishwa na usajili ulio sawa na            njozi za mchana za kumnasa straika wa Real Madrid, Gareth Bale            katika dirisha dogo la Januari.
        Mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham ametajwa katika            orodha ya usajili wa kocha wa Maashetani hao, Louis Van Gaal            ambaye anapambana kuokoa kibarua chake.
        Hata hivyo tayari Real Madrid imekanusha juu ya Bale            kuhamia United ambayo katika siku za hivi karibuni imekuwa            ikihusishwa na usajili wa wachezaji kadhaa wa kadha.
        Mbali Bale, pia United imekuwa ikihusishwa kutaka            kumrejesha kikosini straika wake wa zamani, Cristiano Ronaldo.
        Hata hivyo, mara kadhaa Ronaldo amekuwa akizungumzia            suala la yeye kurejea Old Trafford kuwa ni jambo            linalowezekana, ila linahitaji subira ya kipindi kirefu            kijacho.
        Taarifa za usajili za hivi karibuni zinasema, Bale            amekuwa chaguo la kwanza katika orodha ya usajili wa Old            Trafford huku ikidaiwa kuwa  Van            Gaal anahitaji mchango wa mwanandinga huyo aliyetua Madrid kwa            dau nono la pauni mil. 80.
        Tayari Man United imeweka mezani kitita cha pauni mil.            60 kwa aili ya kumnasa Bale, huku kukiwa na tarifa za kutaka            kuongeza dau zaidi.
        
Comments
Post a Comment