MANCHESTER UINTED YACHUKUA KIPONDO KUTOKA KWA BOURNEMOUTH



MANCHESTER UINTED YACHUKUA KIPONDO KUTOKA KWA BOURNEMOUTH
The            Bournemouth players wheel away in celebration as Spaniard De            Gea lies in the goal after conceding in the second minute

Bournemouth imeichapa Manchester United 2-1 katika mchezo mkali wa Premier League, matokeo yanayozidi kumweka kocha wa United Louis van Gaal kwenye shinikizo kubwa.


Timu hiyo inayoshika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi, wiki iliyopita ilichukua pointi tatu mikononi mwa Chelsea kwa ushindi wa 1-0.

United ilicheza vizuri sehemu ya kiungo na ulinzi japo upande wa kushoto ilipwaya, lakini ni sehemu ya ushambuliaji ndiyo iliyoonekana kikwazo zaidi kwa Van Gaal.

Washambuliaji wa Manchester United walishindwa kabisa kulitia misukosuko ya maana lango la Bournemouth na hata nafasi chache zilizopatikana zilipotea kirahisi.

Bournemouth walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya pili tu ya mchezo  kupitia kwa Junior Stanislas aliyepiga kona iliyokwenda moja kwa moja wavuni huku kipa David de Gea akiishia kuugusa mpira kwa ncha za vidole.


United ikapambana na kusawazisha dakika ya 24 kwa bao la kulazimisha lililotokana na juhudi binafsi za Marouane Fellaini.

Hata hivyo sikio la kufa halisikii dawa, dakika ya 54 Josh King aliyewahi kuichezea Manchester United, akaisulubu timu yake ya zamani kwa kuifungia Bournemouth bao la pili na kumsha shangwe kwenye uwanja uliokuwa na watazamani 11,334.

BOURNEMOUTH: Boruc, Smith, Francis, Cook, Daniels, Surman, Ritchie, Arter (O'Kane 86), Gosling, Stanislas, King (Murray 65)

MANCHESTER UNITED: De Gea, Varela, McNair (Jones 91), Blind, Jackson, Fellaini (Powell 74), Carrick, Mata, Depay, Lingard (Pereira 31), Martial
Former Manchester United                  striker Josh King slides on the turf in celebration                  after regaining Bournemouth's lead against his old club
Mchezaji wa zamani wa Manchester United  Josh King akishangilia bao lake aliloifungia Bournemouth
The Bournemouth players                  congratulate Junior Stanislas (centre) after the hosts                  took a surprise lead in bizarre fashion on Saturday                  night
Wachezaji wa Bournemouth wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na  Junior Stanislas (katikati) 
The former Burnley winger                  whipped in a delivery which flew over Manchester United                  goalkeeper David de Gea and into the top corner
 Junior Stanislas alipiga kona iliyosindikizwa kwenda wavuni na kipa wa United David de Gea
The visitors were soon level                  when Red Devils' Marouane Fellaini tapped home from                  close range in the first half at the Vitality Stadium
Marouane Fellaini anaisawazishia United kwenye dimba la Vitality Stadium
Fellaini is congratulated by                  United team-mate Jesse Lingard after the former Everton                  star levelled the scores in Bournemouth
Fellaini akipongezwa na mchezaji mwenzake Jesse Lingard 







Comments