Bournemouth imeichapa Manchester United 2-1 katika mchezo mkali wa Premier League, matokeo yanayozidi kumweka kocha wa United Louis van Gaal kwenye shinikizo kubwa.
Timu hiyo            inayoshika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi, wiki iliyopita            ilichukua pointi tatu mikononi mwa Chelsea kwa ushindi wa 1-0.
        United            ilicheza vizuri sehemu ya kiungo na ulinzi japo upande wa            kushoto ilipwaya, lakini ni sehemu ya ushambuliaji ndiyo            iliyoonekana kikwazo zaidi kwa Van Gaal.
        Washambuliaji            wa Manchester United walishindwa kabisa kulitia misukosuko ya            maana lango la Bournemouth              na hata nafasi chache zilizopatikana zilipotea kirahisi.
        Bournemouth walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya pili tu ya mchezo kupitia kwa Junior Stanislas aliyepiga kona iliyokwenda moja kwa moja wavuni huku kipa David de Gea akiishia kuugusa mpira kwa ncha za vidole.
United              ikapambana na kusawazisha dakika ya 24 kwa bao la              kulazimisha lililotokana na juhudi binafsi za Marouane                Fellaini.
        Hata hivyo sikio la kufa              halisikii dawa, dakika ya 54 Josh                King aliyewahi kuichezea Manchester United, akaisulubu                timu yake ya zamani kwa kuifungia Bournemouth bao la pili            na kumsha shangwe kwenye uwanja uliokuwa na watazamani 11,334.
        BOURNEMOUTH: Boruc, Smith,            Francis, Cook, Daniels, Surman, Ritchie, Arter (O'Kane 86),            Gosling, Stanislas, King (Murray 65)
        MANCHESTER UNITED: De Gea,            Varela, McNair (Jones 91), Blind, Jackson, Fellaini (Powell            74), Carrick, Mata, Depay, Lingard (Pereira 31), Martial
        Mchezaji wa zamani wa              Manchester United  Josh King akishangilia bao lake              aliloifungia Bournemouth
        Wachezaji wa              Bournemouth wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na               Junior Stanislas (katikati) 
         Junior Stanislas              alipiga kona iliyosindikizwa kwenda wavuni na kipa wa United              David de Gea
        Marouane Fellaini              anaisawazishia United kwenye dimba la Vitality Stadium
        Fellaini akipongezwa na              mchezaji mwenzake Jesse Lingard 
          
Comments
Post a Comment