Wilfried Bony amefunga bao moja dakika ya 26 dhidi ya            timu yake ya zamani Swansea City na kuchangia kuipa Manchester            City pointi tatu muhimu kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England.
        Katika mchezo huo uliochezwa Etihad Stadium, City            imevuna kwa mbinde ushindi wa bao 2-1 huku Swansea ikijilaumu            yenye kupoteza mechi hiyo baada ya kusawazisha dakika ya 90.
        Bafetimbi Gomis aliifungia bao Swansea ambalo            lingewafanya waambulie pointi moja, lakini kabla hawajamaliza            furaha yao, Yaya Toure akaifungia Manchester City ndani ya            dakika tatu za majeruhi.
        Ushindi huo umeifanya Manchester City irejee kileleni            mwa Ligi Kuu kwa pointi 32 na kuishusha Leicester City kwa            tofauti ya magoli.
        Leicester City ambayo nayo ina pointi 32 itakuwa na            kibarua cha kusaka tena nafasi ya kwanza wakati itakapomenyana            na Chelsea Jumatatu usiku.
        Arsenal yenye pointi 30 nayo itakuwa na nafasi nzuri ya            kuongoza ligi iwapo itainyuka Aston Villa Jumapili jioni.
        Matokeo ya mechi zote zilizochezwa Jumamosi jioni              ni:
        Norwich City 1 - 1 Everton
        Crystal Palace 1 - 0 Southampton
        Manchester City 2 - 1 Swansea City
        Sunderland 0 - 1 Watford
        West Ham United 0 - 0 Stoke City
        
Comments
Post a Comment