LIONEL MESSI AICHEZEA BARCELONA MCHEZO WA 500 KWA USHINDI WA KISHINDO ...Suarez hazuiliki, Neymar akosa penalti
Huu ulikuwa ni            usiku wa kihistoria Nou Camp kwa sababu kadha wa kadha -            lakini moja itakayokumbukwa zaidi ni ya Lionel Mess kuichezea            Barcelona mchezo wa 500.
        Barcelona pia            ikawaonyesha mashabiki wake waliojazana Nou Camp mataji matano            waliyotwaa mwaka huu ikiwemo ya Klabu Bingwa ya Dunia kabla            hawajafunga magoli yaliyovunja rekodi ya Real Madrid kwa            kufikisha magoli 18o kwa mwaka mzima. Real Madrid walikuwa            wanashikilia rekodi hiyo kwa magoli 178.
        Messi hakukubali            kusherehekea mchezo wake wa 500 bila kutikisa nyavu ambapo            dakika ya 33 alifunga bao na kuifanya Barcelona iwe mbele kwa            magoli 2-0 kufutia lile la kujifunga la Heiko Westermann dakika ya 29.
        Heiko Westermann alijifunga katika juhudi za kuokoa            mpira  sekunde            chache baada ya Neymar kukosa penalti iliyogonga mwamba na            mpira kurejea uwanjani na ambapo Ivan Rakitic            aliukimbilia kabla hajamgonga Westermann na kujaa wavuni.
        Luis Suarez naye hakubaki nyuma, akatupia wavuni            mabao mawili katika dakika ya 46 na 83 na kuihakikishia            ushindi Barcelona yenye kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi            tatu.
        BARCELONA: Bravo            6.5, Alves 7.5, Vermaelen 7, Mascherano 7, Mathieu 6.5            (Adriano 67, 7), Busquets 8.5 (Bartra 57, 6), Rakitic 7, Sergi            Roberto 8 (Munir 86), Messi 9, Suarez 9.5, Neymar 9 
        REAL BETIS: Adan 9, Molinero            7, Bruno 6 (Pezzella 17), Westermann 6.5 (Digard 36), Vargas            7, N'Diaye 5.5, Petros 6, Cejudo 6.5, Dani Ceballos 8, Van            Wolfswinkel 6, Ruben Castro 6 (Van der Vaart 75) 
        Lionel Messi akicheza              mchezo wake wa 500 kwa Barcelona Jumatano usiku katika              ushindi wa La Liga dhidi ya Real Betis
        Barcelona walizawadiwa              penalti baada ya kipa Antonio Adan kugongana na Lionel Messi              wakati wakiwania mpira
        Neymar alikosa penalti              lakini Ivan Rakitic (kushoto) akawa mwepesi kuchukua hatua              kabla mpira haujamgonga Heiko Westermann na kuwa bao la              kujifunga
        Suarez akiifungia              Barcelona bao la nne
           Barcelona ikipozi na              mataji yake matano iliyotwaa mwaka huu - La Liga, Copa del              Rey, Champions League, European Super Cup na World Club Cup
          
Comments
Post a Comment