LIONEL MESSI AICHEZEA BARCELONA MCHEZO WA 500 KWA USHINDI WA KISHINDO ...Suarez hazuiliki, Neymar akosa penalti


LIONEL MESSI AICHEZEA BARCELONA MCHEZO WA 500 KWA USHINDI WA KISHINDO ...Suarez hazuiliki, Neymar akosa penalti
After            linking up with Neymar, Messi continued his run into the box            and guided his right-footed shot into the bottom corner of the            goal

Huu ulikuwa ni usiku wa kihistoria Nou Camp kwa sababu kadha wa kadha - lakini moja itakayokumbukwa zaidi ni ya Lionel Mess kuichezea Barcelona mchezo wa 500.

Barcelona pia ikawaonyesha mashabiki wake waliojazana Nou Camp mataji matano waliyotwaa mwaka huu ikiwemo ya Klabu Bingwa ya Dunia kabla hawajafunga magoli yaliyovunja rekodi ya Real Madrid kwa kufikisha magoli 18o kwa mwaka mzima. Real Madrid walikuwa wanashikilia rekodi hiyo kwa magoli 178.

Messi hakukubali kusherehekea mchezo wake wa 500 bila kutikisa nyavu ambapo dakika ya 33 alifunga bao na kuifanya Barcelona iwe mbele kwa magoli 2-0 kufutia lile la kujifunga la Heiko Westermann dakika ya 29.

Heiko Westermann alijifunga katika juhudi za kuokoa mpira  sekunde chache baada ya Neymar kukosa penalti iliyogonga mwamba na mpira kurejea uwanjani na ambapo Ivan Rakitic aliukimbilia kabla hajamgonga Westermann na kujaa wavuni.

Luis Suarez naye hakubaki nyuma, akatupia wavuni mabao mawili katika dakika ya 46 na 83 na kuihakikishia ushindi Barcelona yenye kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi tatu.

BARCELONA: Bravo 6.5, Alves 7.5, Vermaelen 7, Mascherano 7, Mathieu 6.5 (Adriano 67, 7), Busquets 8.5 (Bartra 57, 6), Rakitic 7, Sergi Roberto 8 (Munir 86), Messi 9, Suarez 9.5, Neymar 9 

REAL BETIS: Adan 9, Molinero 7, Bruno 6 (Pezzella 17), Westermann 6.5 (Digard 36), Vargas 7, N'Diaye 5.5, Petros 6, Cejudo 6.5, Dani Ceballos 8, Van Wolfswinkel 6, Ruben Castro 6 (Van der Vaart 75) 
Lionel Messi, making his                  500th appearance for Barcelona on Wednesday night,                  starred in his side's La Liga victory over Real Betis
Lionel Messi akicheza mchezo wake wa 500 kwa Barcelona Jumatano usiku katika ushindi wa La Liga dhidi ya Real Betis
Barcelona were awarded                  fortunate penalty in the first half when goalkeeper                  Antonio Adan collided with Lionel Messi after winning                  the ball
Barcelona walizawadiwa penalti baada ya kipa Antonio Adan kugongana na Lionel Messi wakati wakiwania mpira
Neymar missed resulting                  penalty but Ivan Rakitic (left) was first to react                  before the ball rebounded off Heiko Westermann into his                  own net
Neymar alikosa penalti lakini Ivan Rakitic (kushoto) akawa mwepesi kuchukua hatua kabla mpira haujamgonga Heiko Westermann na kuwa bao la kujifunga
Barcelona superstar Messi                  wheels away to celebrate after linking up well with                  Neymar to score his side's second goal of the matchSupastaa wa Barcelona akikimbia kushangilia bao lake
Suarez joined in on the act                  just a minute after the restart to add a third goal for                  Barcelona in Wednesday's La Liga clashSuarez anaendelea kung'ara La Liga kwa kutupia mabao nyavuni
The 28-year-old striker                  added further gloss to the scoreline by doubling his                  tally with a right-footed finish late in the second                  half 
Suarez akiifungia Barcelona bao la nne
Ahead of the tie, Barcelona posed with the La Liga,                  Copa del Rey, Champions League, European Super Cup and                  World Club Cup trophies
 Barcelona ikipozi na mataji yake matano iliyotwaa mwaka huu - La Liga, Copa del Rey, Champions League, European Super Cup na World Club Cup



Comments