LEICESTER CITY YAIKOMALIA MANCHESTER CITY ...sare yao ya 0-0 yaendelea kuiweka Asrenal kileleni



LEICESTER CITY YAIKOMALIA MANCHESTER CITY ...sare yao ya 0-0 yaendelea kuiweka Asrenal kileleni
City            winger Raheem Sterling (right), sporting a new hairstyle,            attempts to wrestle away from the clutches of Danny Simpson
Leicester imeshindwa kukanyaga mwaka 2016 ikiwa kileleni mwa Premier League baada ya kulazimishwa sare ya 0-0 na Manchester City.

Ilikuwa ni mechi ngumu iliyoshuhudia miamba miwili inayowania taji ikichuana vilivyo huku kipa wa Manchester City Joe Hart akilazimika kuokoa katika namna ya kuvutia shuti la Christian Fuchs kunako dakika ya 77.

Sare ni matokeo yaliyosyahili ingawa kwa Leicester ni kama ushindi kwao kutokana na namna wengi walivyobashiri kuwa mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Liverpool wikiendi iliyopita, basi anguko lao limefika.

Matokeo hayo yamekuwa ni mazuri kwa Arsenal ambayo inaendelea kuongoza ligi kwa tofauti ya magoli huku ikiwa imelingana pointi na Leicester inayobakia nafasi ya pili.

LEICESTER CITY: Schmeichel, Simpson, Huth, Morgan, Fuchs, Inler (Ulloa 67), Drinkwater (King 80), Kante, Mahrez, Vardy, Albrighton (De Laet 92)

MANCHESTER CITY: Hart, Sagna, Otamendi, Mangala, Kolarov, Silva (Navas 74), Fernandinho, Toure, Sterling (Iheanacho 88), De Bruyne, Aguero (Bony 64)
Argentina international                  Sergio Aguero watches on with horror as he sees his near                  post flick shoot over the bar from close range
Sergio Aguero kama haamini macho yake kuwa shuti lake limetoka nje
Jamie Vardy (left) was                  slipped through after Fernandinho was robbed deep in his                  own half but the Leicester striker sent his shot overJamie Vardy (kushoto) akiachia shuti kuelekea lango la Manchester City
Marc Albrighton (on the                  floor) could only hit the side-netting as he slid in to                  connect with a Christian Fuchs cross at the back post
Marc Albrighton (aliyelala chini) anashuhudia mpira aliopigia ukigonga nyavu za nje
Raheem Sterling (right)                  watches on as his low effort is tipped agonisingly wide                  of the post by Leicester shot-stopper Kasper Schmeichel
Raheem Sterling (kulia) akiangalia juhudi zake zikizimwa na kipa wa Leicester Kasper Schmeichel
There was concern for Riyad                  Mahrez (centre) after he was hit with a crunching                  challenge by Argentine defender Nicolas Otamendi
 Riyad Mahrez (katikati) akifanyiwa rafu na beki Nicolas Otamendi
Aguero thought he should                  have had a penalty when he was challenged in the box by                  Gokhan Inler but the referee didn't agree
Aguero anaamini alistahili kupewa penalti baada ya kuchezewa rafu na Gokhan Inler ndani ya box lakini refari akaipotezea



Comments