LEICESTER CITY YAIKALISHA CHELSEA 2 - 1 …Mourinho hali tete, Arsenal yashushwa


LEICESTER CITY YAIKALISHA CHELSEA 2 - 1 …Mourinho hali tete, Arsenal yashushwa

Licha ya kukingiwa kifua na mmiliki wa timu, mashabiki na wachambuzi kibao wa soka, kibarua cha Jose Mourinho si salama.

Chelsea imechukua kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Leicester City  kwenye mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa Jumatatu usiku, matokeo ambayo yanaishusha Arsenal hadi nafasi ya pili.

Leicester City  inayonolewa na kocha wa zamani wa Chelsea, Claudio Ranieri, imedhihirisha kuwa haina mpango wa kuwa msindikizaji bali ni klabu iliyopania kutwaa taji la Premier League.

Mshambuliaji anayewatesa walinda milango, Jamie Vardy aliunganisha krosi ya Riyad Mahrez Leicester bao kwanza dakika ya 34 na kudumu hadi mapumziko.

Dakika ya 48 Riyad Mahrez akapachika bao la pili kwa wenyeji kabla ya Loic Remy hajafungia Chelsea goli la kufutia machozi dakika ya 77.

Leicester City  inangoza ligi kwa pointi 35 ikifuatiwa na  Arsenal yenye pointi 33, Manchester City ni ya tatu kwa pointi zake 32 wakati Manchester United ikikamata nafasi ya nne kwa pointi 29.

LEICESTER CITY (4-4-1-1): Schmeichel 7, Simpson 6.5, Morgan 7, Huth 7, Fuchs 7, Mahrez 8.5 (Inler 82), Drinkwater 5 (King 17, 6), Kante 8, Albrighton 7, Ulloa 7, Vardy 8 (Okazaki 88). 


CHELSEA (4-2-3-1): Courtois 6.5, Ivanovic 6, Zouma 5, Terry 4.5 (Fabregas 53, 5), Azpilicueta 5, Ramires 5, Matic 6, Willian 6, Oscar 6 (Remy 65, 7), Hazard 5 (Pedro 30, 6.5), Costa 5.
Chelsea were frustrated by                  Leicester on Monday night - with the Foxes now on top of                  the Premier League after the victory
Chelsea wakiwa hoi wakati wakizamishwa kwenye mchezo wa Premier League 
Jamie Vardy celebrates                    after scoring the opening goal of the Premier League                    game against Chelsea on Monday night
Jamie Vardy akishangilia bao la kwanza
The in-form striker made a run in between John                      Terry and Kurt Zouma to volley in his 15th goal of                      the season in the 34th minuteJamie Vardy akifunga bao lake la 15 msimu huu baada ya kuwazidi maarifa John Terry na Kurt Zouma
Riyad Mahrez doubled                    Leicester's advantage against the champions with his                    12th of the campaign early on in the second half
Riyad Mahrez akishangilia bao la pili la Leicester City
Loic Remy gave Chelsea                        a lifeline with a header from close range with                        Kasper Schmeichel unable to stop himLoic Remy akiifungia Chelsea bao pekee huku kipa  Kasper Schmeichel akiwa hana la kufanya



Comments