Licha ya mwendo wa kusuasua, kocha wa Liverpool, Jurgen            Klopp amesema kwamba amejipanga vyema na kamwe haoni kama kuna            timu yoyote inawatisha katika michuano mbalimbali            inayowakabili.
        Klopp aliyasema hayo wakati akiongea na waandishi wa            habari na kudai kuwa amegundua kikosi chake kiko vizuri licha            ya kuwepo kwa kasoro kadhaa hasa upande wa ushambuliaji ambapo            wamekuwa wanapoteza nafasi nyingi za kupachika mabao.
        Alisema, hakuna timu yoyote ambayo inampa presha hivi            sasa kwenye michuano ya Ligi Kuu na michuano mingine  kwa vile            vijana wake wapo sawasawa licha ya kukabiliana na upinzani            mkali.
        "Sitishwi na timu yoyote, tupo makini kufanya vema            katika michuano inayotukabili," alisema kocha huyo.
        
Comments
Post a Comment