Baada ya mwendo mzuri chini ya kocha mpya Jurgen Klopp hatimaye Liverpool imekwaa kisiki kwa kunyukwa 2-0 na Newcastle kwenye mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa St James Park Jumapili jioni.
Magoli ya Newcastle inayoshika nafasi ya tatu kutoka chini, yalitokana na juhudi za kiungo Georgino Wijnaldum aliyesababisha goli la kwanza dakika ya 69 baada ya shuti lake kumgonga beki Martin Skrtel na kwenda wavuni kabla hajafunga bao la pili dakika ya 90.
Newcastle (4-2-3-1): Elliot 6; Janmaat 7.5, Mbemba 7, Coloccini 7, Dummett 7.5; Colback 6.5 (Gouffran 77, 6), Anita 8; Sissoko 6.5, De Jong 5.5 (Perez 68, 6), Wijnaldum 8.5; Cisse 6.5 (Thauvin 82, 6)
Liverpool (4-2-3-1): Mignolet 6; Clyne 6.5, Skrtel 5, Lovren 5, Moreno 6.5; Lucas 6, Allen 6; Milner 5.5, Firmino 5 (Sturridge 62, 6), Ibe 6.5 (Origi 75, 5); Benteke 4.5 (Lallana 62, 6)
Shuti la dakika ya 69 la Wijnaldum linagonga mguu wa beki wa Liverpool Martin Skrtel (kulia) na kuisababishia Newcastle ipate bao la kwanza
Comments
Post a Comment