Jose Mourinho yupo tayari, tena mwenye            utashi kupita maelezo ya kumrithi Louis van Gaal iwapo kocha            huyo wa Uholanzi atatimuliwa Manchester United.
        Kibarua Van Gaal            kiko hatarini baada ya mwendo mbovu uliopekelea Manchester            United kushinda mechi tatu tu katika michezo yake 13 ya mwisho            katika mashindano yote.
        Jose Mourinho            alitimuliwa Chelsea katikati ya wiki iliyopita na sasa nafasi            iko wazi kwake kujiunga na Manchester United iwapo Van Gaal            atafungasha virago.
        Licha ya bodi ya            Manchester United kumpa kura ya imani Van Gaal huko nyuma,            lakini kipigo cha 2-1 kutoka kwa Norwich Jumamosi iliyopita            kwenye mchezo wa Ligi Kuu, kimeamsha wasiwasi wa maisha ya            kocha huyo Old Trafford.
        Van Gaal mwenyewe            amekiri kuwa sasa anaanza kuhofia kibarua chake Manchester            United na kukiri kuwa iwapo timu haitaanza kushinda basi            atakuwa hayuko salama.
        Jose Mourinho (katikati              kushoto) yupo tayari kumrithi Van Gaal iwapo atatimuliwa
        Mourinho huenda              akamrithi Van Gaal
        Van Gaal hati hati              Manchester United 
        
Comments
Post a Comment