JOSE MOURINHO YUPO TAYARI KUMRITHI VAN GAAL MANCHESTER UNITED



JOSE MOURINHO YUPO TAYARI KUMRITHI VAN GAAL MANCHESTER UNITED
Jose Mourinho yupo tayari, tena mwenye utashi kupita maelezo ya kumrithi Louis van Gaal iwapo kocha huyo wa Uholanzi atatimuliwa Manchester United.


Kibarua Van Gaal kiko hatarini baada ya mwendo mbovu uliopekelea Manchester United kushinda mechi tatu tu katika michezo yake 13 ya mwisho katika mashindano yote.

Jose Mourinho alitimuliwa Chelsea katikati ya wiki iliyopita na sasa nafasi iko wazi kwake kujiunga na Manchester United iwapo Van Gaal atafungasha virago.

Licha ya bodi ya Manchester United kumpa kura ya imani Van Gaal huko nyuma, lakini kipigo cha 2-1 kutoka kwa Norwich Jumamosi iliyopita kwenye mchezo wa Ligi Kuu, kimeamsha wasiwasi wa maisha ya kocha huyo Old Trafford.

Van Gaal mwenyewe amekiri kuwa sasa anaanza kuhofia kibarua chake Manchester United na kukiri kuwa iwapo timu haitaanza kushinda basi atakuwa hayuko salama.

Jose Mourinho (centre left)                  is ready and willing to replace Louis van Gaal if he is                  sacked by Manchester United
Jose Mourinho (katikati kushoto) yupo tayari kumrithi Van Gaal iwapo atatimuliwa
Mourinho, pictured walking                    near his house on Sunday morning, would jump at the                    chance to replace Van Gaal     Mourinho was sacked by                    Chelsea last week
Mourinho huenda akamrithi Van Gaal
Van Gaal oversaw another                  defeat as Manchester United boss on Saturday and his                  side have won three in 13
Van Gaal hati hati Manchester United 


Comments