JOSE MOURINHO ASEMA JAMIE VARDY ANAWEZA KUNG’ARA KWENYE KLABU YOYOTE DUNIANI


JOSE MOURINHO ASEMA JAMIE VARDY ANAWEZA KUNG'ARA KWENYE KLABU YOYOTE DUNIANI
Jamie Vardy (right)            scores during Leicester's 2-1 win over Chelsea at the King            Power Stadium on Monday
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema kuwa mshambuliaji wa Leicester City, Jamie Vardy (pichani kulia) ana ubora wa kucheza klabu yoyote duniani.

Mshambuliaji huyo kwa sasa anaongoza kwa upachikaji mabao katika michuano ya Ligi Kuu England, ambapo hadi sasa ana jumla ya mabao 14 huku akifuatiwa na mshambuliaji wa Everton, Lumelu Lukaku mwenye mabao 12.

Kutokana na uwezo wa Vardy, Mourinho anaamini kuwa mchezaji huyo anaweza kupata mafanikio katika klabu yoyote.

"Kwa sasa yeye ni mchezaji ambaye anaongoza kwa kufunga mabao, ninaamini hakuna klabu abayo haimkubali mchezai huyo. 

"Kutokana na uwezo wake, ninaamini anaweza kucheza klabu yoyote duniani na kupata mafanikio makubwa kama ilivyo kwa nyota wengine," alisema Mourinho.

Vardy mwenye umri wa miaka 28 alivunja rekodi ya kupachika mabao 11 katika michezo 11 ya mwanzoni mwa michuano ya Ligi Kuu nchini England hivyo Mourinho anaamini msimu ujao hakuna mchezaji ambaye anaweza kuvunja rekodi ya mchezaji huyo.


"Ameweka rekodi ya aina yake, sina hakika kama kuna mchezaji ambaye anaweza kupachika mabao 11 katika michezo ya mwanzoni na kuvunja rekodi yake, itakuwa ni ndoto," alisema Mourinho.


Comments