Kipa wa Manchester            City Joe Hart amesisitiza kuwa timu yao ilistahili kuwa            kileleni mwa Premier League katika kipindi hiki ambacho ligi            imefikia katikati ya msimu.
        Kikosi cha Manuel            Pellegrini kinashika nafasi ya tatu kikiwa nyuma kwa pointi            tatu dhidi ya vinara Arsenal na hiyo ni baada ya kuambulia            sare ya 0-0 kwa Leicester inayoshika nafasi ya pili.
        Golikipa huyo namba            moja wa England alifanikiwa kulinda vema lango lake kutoka kwa            wafungaji wenye uchu Riyad Mahrez na Jamie Vardy, lakini            anaamini  City ilistahili kuondoka na pointi tatu King Power            Stadium kutokana na nafasi  walizozitengeneza.
        Joe                Hart anasema  Manchester City ilistahili kuongoza ligi
          "Hatupo sehemu            tunayostahili, hii  ni kutokana na kutocheza vema katika            baadhi ya michezo yetu," Hart aliiambia tovuti ya Manchester            City.
        "Tulianza msimu kwa            nguvu lakini hatukucheza vizuri katika mechi 12 za mwisho ila            tuko kwenye nafasi nzuri na timu zote mbili zilizoko juu yetu            zimestahili kuwa hapo.
        "Bila shaka yoyote,            ili tuwe juu tunalazimika kushinda - kushinda mechi zote za            nyumbani na kukomaa ili kushinda pia michezo ya ugenini"
        Msimamo wa ligi                ukionyesha top six
          Joe                Hart akipangua shuti la Riyad Mahrez (kulia) 
          
Comments
Post a Comment