Kocha huyo amehoji            iwapo kweli wachezaji wake wanaonyesha uwajibikaji wa kweli            baada ya kipigo cha tisa msimu huu na kubakia pointi moja tu            juu ya janga la kushuka daraja.
        Aidha, Mourinho              pia amehoji uwajibikaji wa  Eden              Hazard baada ya nyota huyo wa              kimataifa wa Ubelgiji kujiondoa mwenyewe dimbani kwa madai              ya kuumia paja kipindi cha kwanza.
        Leicester walicheza            soka bab kubwa na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu kupitia magoli            ya Jamie Vardy na Riyad Mahrez ambao kwa pamoja wana jumla ya            magoli 26 katika Premier League msimu huu. 
        Licha ya Loic Remy            kuifungia Chelsea bao pekee dakika ya 77, lakini bado timu            hiyo haikuonyesha mapambano ya dhati ya kusaka pointi katika            kipindi hiki ambacho Mourinho anapigania kibarua chake kwa            kila hali.
        "Ninahisi kazi            yangu inasalitiwa," alisema Mourinho. "Tuliruhusu magoli            mawili katika namna ambayo kwangu inanipa mashaka.
        "Najua kuwa moja ya            ubora wangu ni namna ya kuusoma mchezo kwa wachezaji wangu,            kusoma wapinzani na kubaini tishio kutoka kwa wapinzani wetu. 
        "Vardy alikwenda              katikati ya mabeki wawili wa kati na kufunga bao la kwanza, Mahrez  akawa na mtu              mmoja kwenye box lakini mimi nataka watu wawili. Nahitaji              mchezaji wa kiungo akabe ipasavyo. Aina ya magoli mawili              tuliyofungwa ni jambo gumu kulipokea.
          
"Mechi hii niliifanyia kazi kwa siku nne. Nilifundisha kila kitu kuhusiana na wapinzani wetu. Nikataja nyendo zao nne za hatari ambazo ndizo walizotumia kwa kiasi kikubwa kufunga kila bao dhidi yetu.
          
"Wachezaji wangu walipata maelekezo yote mazoezini ndani ya siku tatu za mwisho. Unaweza kuwauliza wao. Najua ni waungwana na watakuambia ninachosema ni ukweli mtupu."
        "Mechi hii niliifanyia kazi kwa siku nne. Nilifundisha kila kitu kuhusiana na wapinzani wetu. Nikataja nyendo zao nne za hatari ambazo ndizo walizotumia kwa kiasi kikubwa kufunga kila bao dhidi yetu.
"Wachezaji wangu walipata maelekezo yote mazoezini ndani ya siku tatu za mwisho. Unaweza kuwauliza wao. Najua ni waungwana na watakuambia ninachosema ni ukweli mtupu."
Kocha wa Chelsea  Jose Mourinho              akishangaa kwenye mchezo wa Premier League dhidi ya              Leicester
        Jamie Vardy anashangilia bao lake dhidi              ya Chelsea
        
Comments
Post a Comment